IQNA

Mkuu wa Al-Azhar yuko Bahrain kwa Mkutano wa Mazungumzo ya Kiislamu 

15:10 - February 20, 2025
Habari ID: 3480243
IQNA - Imamu wa Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar cha Misri, Sheikh Ahmed al-Tayeb amesafiri kwenda Bahrain kushiriki mkutano wa kimataifa wa mazungumzo ya Kiislamu.

Amehutubia sherehe za ufunguzi wa mkutano huo, unaofanyika Manama tarehe 19-20 Februari.

Uliopewa jina la “Taifa Moja, Hatima ya Pamoja”, mkutano huo umeandaliwa kwa pamoja na Kituo cha Al-Azhar, Baraza Kuu la Masuala ya Kiislamu huko Bahrain, na Baraza la Wazee wa Kiislamu.

Umeleta pamoja wasomi wa Kiislamu zaidi ya 400, viongozi, wasomi na wataalamu kutoka kote ulimwenguni.

Mkutano huo unasisitiza umuhimu wa kuimarisha msingi wa pamoja kati ya Waislamu na kuunganisha juhudi za kukabiliana na changamoto za sasa, kwa njia inayosaidia kufikia mshikamano mkubwa na ujumuishaji kati ya mataifa ya Kiislamu.

Pia unafanyika kwa lengo la kuimarisha mazungumzo ya Kiislamu na kuunganisha maadili ya kuelewana na kukaribiana kati ya vipengele vya Umma wa Kiislamu. Kwa kusudi hili, masuala na changamoto kuu zinajadiliwa, zikisisitiza umuhimu kutazama uwepo wa mitazamo tofauti kama chanzo cha nguvu na umoja kati ya Waislamu.

Mkutano huo pia unalenga kuamsha jukumu la mamlaka na taasisi za kidini na kisayansi katika kukuza fikra za wastani, kusaidia katika kushughulikia changamoto za umoja wa Kiislamu, na kuendeleza mpango wa kudumu wa kuchochea mazungumzo ya Kiislamu na kutatua tofauti.

Kutoka Iran, Hujjatul-Islam Hamid Shahriari, katibu mkuu wa Jukwaa la Ulimwengu la Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu, ameshiriki katika mkutano huo.

 3491923

Habari zinazohusiana
captcha